Nigeria:Watu 29 wauawa msikitini
Watu 29 wameuawa katika mji wa Maiduguri Watu 29 wameuawa kati mji mkuu wa jimbo la Borno Maiduguri Kaskazini Mashariki mwa Nigeria baada ya mlipuaji wa kujitoa mhanga kujilipua ndani ya msikiti. Kamishna wa polisi katika jimbo la Borno amesema kuwa watu wengine 28 walijeruhiwa kwenye shambulizi hilo. Shambulizi hilo lilifuatia jaribio la awali la kuuteka ya mji wa Maiduguri lililondeshwa na wanamgambo wa kiislamu wa Boko Haram. Wanagamabo hao walifyatua makombora kwenye makazi ya watu na kuua takriban watu 13. Rais Buhari ameapa kukabiliana kikamilifu na wapiganaji wa Boko Haram Siku ya ijumaa rais mpya wa Nigeria Muhammadu Buhari aliahidi wakati wa kuapishwa kwake kuwa atakabiliana vilivyo na kundi hilo la wapiganaji wa Boko Haram. Rais Buhari alisema kuwa kituo cha kijeshi kitawekwa katika mji wa Maiduguri kusadia kupigana na wanamgambo hao. Rais Buhari akihutubia taifa punde baada ya kuapishwa alisema kuwa jeshi la taifa hilo litakita kambi yake katika mji huo wa...