Jumuiya ya kimataifa inaelekea kukosa uvumilivu..

Viongozi wanaosimamia zoezi la usitishwaji mapigano nchini Sudani Kusini wamevionya vikosi vya pande mbili zinazokinzana nchini humo kuwa jumuiya ya kimataifa inaelekea kukosa uvumilivu kufuatia hatua yao ya kushindwa kutekeleza mkataba wa amani walioutia saini miezi 7 iliyopita.
Mkuu wa ujumbe unaosimamia utekelezwaji wa makubaliano ya amani, rais wa zamani wa Botswana, Festus Mogae, amesema timu yake itahakikisha mkataba huo wa amani uliotiswa saini mwezi August mwaka jana unatekelezwa licha ya mapigano kuendelea kushudiwa.
Rais Mogae, amezionya pande hizo na kuongeza kuwa kutotekeleza mkataba wa amani walioutia saini ni kuijaribu jumuiya ya kimataifa na kwamba uvumilivu wake unaelekea kufikia mwisho.


Source:Focusmedia




























































































































Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Wachezaji Ligi Kuu wakatiwa Bima ya Afya...

Orodha ya nchi 10 zaidi duniani zenye idadi kubwa ya watu kuliko nchi nyingine (2000-2015) na Nigeria ikiwa ndio nchi ya pekee kutoka bara la Afrika