MANCHESTER UNITED YAMTUMIA ZAWADI DAVID BECKHAM.
David Beckham anaweza kuwa na mashabiki ambao sio mashabiki wa Manchester united. Hiki kitu kinawezekana kabisa lakini hivi sasa Manchester United wamezindua jezi zao mpya na kampuni ya Adidas.
Manchester wamemtumia mchezaji wao zamani zawaid ya jezi yenye jina lake na namba aliyowai kuchezea akiwa hapo Old Trafford. Zaidi ni kwamba familia nzima ya Beckham ambayo inaishi Marekani imetumia jezi hizo mpya.
Beckham amepost picha kwenye instagram yake yenye mashabiki wengi na kusema kwamba amepewa zawadi hiyo. Hapo kuna mashabiki wa Beckham wanaweza kuwa wamevutiwa na jezi hiyo na kuiongezea biashara club ya Manchester united.
Hapa nyumbani Simba imezindua jezi mpya, pia kuna uwezekano wa kufanya marketing kubwa kwa kuwatumia mashabiki maarufu wa club hiyo kama actor JB, actress Odama na wasanii wa muziki ambao wana mashabiki mbalimbali watakaopata kuzijua jezi za Simba kupitia hao watu.
SOURCE:Shaffihdauda.com
Maoni
Chapisha Maoni