Diamond Platnumz apokea ushindi wa tuzo nyingine mbili za African NAFCA Awards 2015...
Mwaka huu umekuwa mzuri sana kwa mtu wetu Diamond Platnumz kwani amekuwa wa kupokea na kutajwa kwenye tuzo nyingi sana kwa mwaka huu wa 2015 na siku chache zilizopita Diamond Platumz alitajwa kuwania tuzo nyingine tena za kimatatifa MTV EMA 2015 jijini Milan Italy.
Headlines za Diamond Platnumz haziishii hapo, good news kwako mtu wangu msanii wetu wa Bongo Flava anazidi kuonyesha ubora wake kwenye nafasi mbalimbali za tuzoAfrica… Diamond amepokea ushindi wa tuzo nyingine tena! African NAFCA Awards 2015 imemtaja Diamond kuwa Msanii wa mwaka anaependwa na wimbo wa ‘Nana’umetajwa kuwa Wimbo wa mwaka unaopendwa!
Kupita page yao ya Instagram @africannafca walipost picha hizi za tuzo za Diamond Platnumz…
2.Favorite Song of the Year – NANA wa Diamond Platnumz.
Na kupitia page yake ya Instagram, Diamond Platnumz amepost picha ya tuzo zake na ujumbe wa shukrani kwa mashabiki wake…
SOURCE:Millardayo.com
Maoni
Chapisha Maoni