Bodi ya rushwa ya AU yaridhishwa na serikali ya Tanzania katika kudhibiti rushwa...



Wajumbe wa bodi ya kupambana na rushwa kwa nchi za umoja wa Afrika (AU) wameelezea kuridhishwa kwake na misingi iliyowekwa na serikali ya Tanzania ya  kudhibiti vitendo vya rushwa haswa wakati huu wa uchaguzi.

Wakizungumza baada ya kumaliza kikao chao cha kutathmini hatua iliyofikiwa  kukabiliana na rushwa kwa nchi za umoja wa Afrika mwenyekitia wa bodi hiyo   Daniel Batdam amesema pamoja na changamnoto zilizopo hatua iliyofikiwa na  Tanzania katika kukabiliana na rushwa inafaa kuigwa  na  nchi  zingine.
 
Aidha Bw.Batdam ameitaka Tanzania  kuendelea  kuziba  mianya yote ya rushwa  wakati  huu  wa  uchaguzi ili uchaguzi uweze kumalizika  kwa  amani  na kuendelea kuwa  mfano wa nchi za umoja wa Afrika  zenye  hazina  kubwa  ya  amani.
 
Wajumbe wa  bodi  hiyo ambao wamekutana jijini Arusha kwa siku  tano  pia wamejadili masuala  mbalimbali  ya miradi  ya maendeleo  ukiwemo wa uenzi wa makao yake makuu yanayojengwa  hapa nchini  katika  mkoa wa Arusha.








SOURCE:ITV
























Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Imetangazwa noti yenye muonekano mzuri kuliko zote duniani kwa mwaka 2016..

Picha 10 za Ikulu zilizo nzuri zaidi Duniani...